KILE KITAKACHO TUPONZA WATANZANIA
Ni muda mrefu sana toka Tanzania ijipatie
 uhuru wake, pamoja na misukosuko ambayo tulipitia hatuna budi 
kumshukuru Mungu, amani imekuwa ndiyo sifa kubwa ya nchi hii katika 
mataifa mbalimbali duniani, hili limetupelekea kwa namna moja ama 
nyingine kuendelea kiuchumi kupitia sekta ya utalii ambayo kwa sasa 
ndiyo sekta kuu ya pili kuliingizia taifa mapato.
Lakini wasiwasi unazidi kuendelea pale 
ambapo yanatokea mambo mbalimbali ambayo kwa namna moja ama nyingine 
yamekuwa yakituharibia sifa yetu kuu ya kuwa kisiwa cha amani.
Jambo linalonisikitisha zaidi ni pale ambapo watanzania wenyewe tumekuwa mstari wa mbele kuchochea kupoteza sifa yetu hii kuu
Kwnza kabisa 
ningependa kuanza na vyombo vya habari ambavyo kwa namna moja au 
nyingine vina mchango mkubwa sana katika kudumisha amani au hata 
kuipoteza amani.
Kwa siku kadhaa sasa tumekuwa 
tukishuhudia wamiliki wa mitandao mbalimbali ya kijamii wakiandika 
habari kuhusu kuwepo ma mgogro kati ya Tanzania na Rwanda, ikiwemo kutoa
 kauli ambazo kimsingi hazijulikani kuwa vyanzo vyake ni vipi.
Ni kweli kuwa kila mtu ana wajibu wa 
kupata taarifa na kupokea taarifa bila kuzuiwa, lakini pia lazima uwepo 
utaratibu mzuri wa utoaji wa taarifa hizo, la sivyo yanaweza kutukuta 
yale ambayo yaliwapata majirani zetu Kenya mwaka 2007/2008 ambapo vyombo
 ya habari vilikuwa na mchango mkubwa sana katika mgogoro ambao 
uligharimu maisha ya watu wengi.
Mtazaomo wangu ni kwamba, kama hakutakuwa
 na udhibiti katika swala zima ta utoaji wa habar basi tusubiri kwa muda
 usio mrefu na tutajikuwa katika wakati ambao hakuna hata mmoja wetu 
anautegemea wala kuupenda.
Wito wangu kwa Serikali, Vyombo vya habari na Wamiliki wa mitandao hii ya kijamii zikiwemo blogs:
- Tufanye uchunguzi kwanza kwa habari tunazotaka kuzitoa kwa uma ili kuepusha kuwachanganya wananchi ambao kwa namna moja ama nyingine hatuujui ukweli wa mambo.
- Serikali kupitia wizara ya mambo ya habari na mawasiliano iweke utaratimu maalumu wa utoaji na uandikaji wa taarifa katika blog na mitandao mbalimbali ya kijamii.
- Swala zima la utoaji wa kuhusiana na maswala yanayoigusa nchi ziachwe chini ya wizara husika na sio mtu mmoja mmoja kuandika tena vitu ambavyo havina uthibitisho wala uchunguzi wowote.
- Mwisho kabisa napenda kuwasihi watanzania kuacha kushabikia maswala linalohisinana na migogoro, tunatakiwa tujue kwamba zipo sehemu ambazo wanatamani japo kupata amani ya siku moja tu wakapata muda wa kukaa pamoja na familia zao lakini kutokana na machafuko yalitopo inakuwa vigumu sana.
Tukumbuke kwamba kuipoteza amani linaweza kuwa swala la siku moja tu lakini kuirudisha tena likatugahrimu maisha yetu yote.
Ningependa kuona kama sisi tungejifunza 
kupitia majirani zetu ambao wameshapitia katika machafuko na wale ambao 
bado wapo katika machafuko, kupitia wao tuone ni namna gani tutaidumisha
 amani katika nchi yetu Tanzania.
Mimi binafsi naipenda sana nchi yangu 
Tanzania, najivunia sana kuzaliwa katika nchi hii japokuwa yapo 
mapungufu mbalimbali yanayotukabili, hii hainifanyi kuwa mmoja wa wale 
wanaoitakia mabaya nchi yangu, ningependa na nitafurahi sana kama 
watanzania wote tungeungana na kuitakia amani nchi yetu ikiwemo kuiombea
 na kuwapinga vikali wale ambao kwa namna moja ama nyingine wamekuwa 
wanachochea katika kuipoteza amani yetu.
Mungu ibariki Tanzania, Mungu tubariki 
watanzania, amani iwe chetu cheo, fujo kuzikwepa, kwa upendo na 
mshikamano kuishi na udugu wetu wa enzi kuuenzi
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 


 
 
 
 
 
 
No comments
Thank for your coment