TUWASAIDIE WENYE UHITAJI

Huyu ni moja kati ya binti wawili ambao wameamua kujifanyia biashara ya kuuza chakula yaani mamantilie ali maarufu kama (WAJASI) kama wanafunzi wa chuo kikuu cha Dodoma wanavyowaita.
Ni mwaka jana tu walihitimu kidato cha nne ambapo Mary Andrew miaka 17, ambaye yuko picha yeye alipata daraja la 4 kwa alama 28 na mwenzake Vaileth Chusi miaka 18, alipata daraja hilohilo kwa alama 26.
Lakini nilipokuwa nikiongea nao na kuwahoji hasa sababu ya kuamua kujishughulisha na biashara hiyo na nini hasa malengo yao kuhusu kuendelea na elimu,
Vaileth: Sio kuwa tumependa kuwa hapa ila ni kutokanatu na hali ngumu ya maisha ya wazazi wetu, kuwa mahali hapa huwa ni hatari kwetu kwanza wanachuo wanatusumbua sana wakitutaka kimapenzi kitu kinacho tupa wakati mgumu, tunatamani kuendelea na masomo ila basi hatuna uwezo huo.
Mary: Kweli kwa msichana mdogo kama mimi kuwepo mazingira haya huwa yananiumiza ila sina lakufanya.

No comments

Thank for your coment

Powered by Blogger.