Tutakukumbuka Daima

Mshituko mkubwa umewakumba watu wengi, hasa wapenzi wa filamu za Bongo (Bongo Movies). Ni baada ya kuondokewa na mpenzi wao (wetu) muigizaji mahiri katika tasnia hiyo Steven Charles Kanumba maarufu kama "The Great"

Kanumba amefariki usiku wa kuamkia jana jumamosi tarehe 7, Machi 2012, hata hivyo sababu za kifo chake hazijajulikana japokuwa kuna tetesi kuwa amefariki baada ya kuanguka ambapo ameumia sehemu ya kichwa.
Hilo limetokea baada ya kugombana na anayesemekana kuwa mpenzi wake Elizabet Michael maarufu kama "LULU" ambapo alimkuta akiwa anaongea na mtu mwingine kupitia simu yake ya mkononi. Inasemekana ilikuwa yapata saa sita usiku ambapo Kanumba alikuwa ametoka kuonga ili ajiandae waweze kutoka out.

Jeshi la polisi limamshikilia mwanadada huyo ili kulisaidia katika uchunguzi wa tukio hilo.

Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi. Amina.

No comments

Thank for your coment

Powered by Blogger.